Surah Al-Humazah in Swahili

    الهمزة

    Surah Al-Humazah in Swahili

    Read Surah Al-Humazah in Swahili (الهمزة) with Arabic text, Swahili translation, and audio recitation. Chapter 104 of the Holy Quran, 9 verses — free online.

    Quran in Swahili · all 114 Surahs

    1

    وَيۡلٞ لِّكُلِّ هُمَزَةٖ لُّمَزَةٍ

    Ole wake kila safihi, msengenyaji! [1]

    [1] Atapata adhabu kali na maangamio huyo ambaye mtindo wake ni kuwafedhehi watu kwa kauli au kwa ishara, au kuwasengenya kuwavunjia hishima zao.

    2

    ٱلَّذِي جَمَعَ مَالٗا وَعَدَّدَهُۥ

    Aliye kusanya mali na kuyahisabu. [2]

    [2] Ambaye amekusanya chungu ya mali na akawa kazi yake kuyahisabu tu, kwa kuona ladha huko kuhisabu.

    3

    يَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخۡلَدَهُۥ

    Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele! [3]

    [3] Anadhani huyo kuwa mali yake yatamweka milele duniani, na yatamkinga na hayo anayo yachukia?

    4

    كَلَّاۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِي ٱلۡحُطَمَةِ

    Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama. [4]

    [4] Na aache dhana hiyo! Wallahi! Hapana shaka yoyote kwa vitendo vyake viovu hivyo atakuja tumbukizwa katika Moto unao vuruga kila kinacho tupwa humo!

    5

    وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحُطَمَةُ

    Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama? [5]

    [5] Na kitu gani kitacho kujuvya nini ukweli wa Moto huu wa H'ut'ama?

    6

    نَارُ ٱللَّهِ ٱلۡمُوقَدَةُ

    Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa. [6]

    [6] Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa kwa amri yake, na daima unawaka!

    7

    ٱلَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى ٱلۡأَفۡـِٔدَةِ

    Ambao unapanda nyoyoni. [7]

    [7] Ambao unafikilia nyoyoni na kuzizunguka nyoyo.

    8

    إِنَّهَا عَلَيۡهِم مُّؤۡصَدَةٞ

    Hakika huo utafungiwa nao [8]

    [8] Huo utakuwa umefungwa milango yake, na wao watakuwa wamefungwa humo ndani

    9

    فِي عَمَدٖ مُّمَدَّدَةِۭ

    Kwenye nguzo zilio nyooshwa. [9]

    [9] Kwenye maguzo yaliyo nyooka. Hawawezi kutaharaki, wala kutoka.

    Al-Humazah

    Play