Surah Al-Fil in Swahili

    الفيل

    Surah Al-Fil in Swahili

    Read Surah Al-Fil in Swahili (الفيل) with Arabic text, Swahili translation, and audio recitation. Chapter 105 of the Holy Quran, 5 verses — free online.

    Quran in Swahili · all 114 Surahs

    1

    أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصۡحَٰبِ ٱلۡفِيلِ

    Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo? [1]

    [1] Hakika, ewe Muhammad, unajua kwa ujuzi usio ingiliwa na shaka yoyote, alivyo fanya Mola wako Mlezi kuwafanyia wale watu wenye tembo (ndovu), wakataka kuishambulia Nyumba takatifu ya Al-Kaaba.

    2

    أَلَمۡ يَجۡعَلۡ كَيۡدَهُمۡ فِي تَضۡلِيلٖ

    Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? [2]

    [2] Unajua ya kwamba hakika Mwenyezi Mungu amejaalia juhudi yao kutaka kuibomoa Al-Kaaba ivize na ipotelee mbali. Juhudi yao ikapeperuka, na wao wasipate makusudio yao.

    3

    وَأَرۡسَلَ عَلَيۡهِمۡ طَيۡرًا أَبَابِيلَ

    Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi, [3]

    [3] Na Mwenyezi Mungu aliwasalitisha na majeshi ya ndege yaliyo watokea makundi kwa makundi yakifuatana, na yakawazunguka kila upande.

    4

    تَرۡمِيهِم بِحِجَارَةٖ مِّن سِجِّيلٖ

    Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni, [4]

    [4] Wakiwatupia mawe kutoka Jahannamu.

    5

    فَجَعَلَهُمۡ كَعَصۡفٖ مَّأۡكُولِۭ

    Akawafanya kama majani yaliyo liwa! [5]

    [5] Akawafanya kama majani ya mimea yaliyo sibiwa yakatilifu.

    Al-Fil

    Play