وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيۡتُونِ
Naapa kwa tini na zaituni! [1]
[1] Naapa kwa tini na zaituni, kwa baraka zao na ubora wa manufaa yao.
التين
Read Surah At-Tin in Swahili (التين) with Arabic text, Swahili translation, and audio recitation. Chapter 95 of the Holy Quran, 8 verses — free online.
Quran in Swahili · all 114 Surahs
وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيۡتُونِ
Naapa kwa tini na zaituni! [1]
[1] Naapa kwa tini na zaituni, kwa baraka zao na ubora wa manufaa yao.
وَطُورِ سِينِينَ
Na kwa Mlima wa Sinai! [2]
[2] Na kwa mlima ambao juu yake ndio Mwenyezi Mungu alimsemeza Musa.
وَهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ ٱلۡأَمِينِ
Na kwa mji huu wenye amani! [3]
[3] Na kwa huu mji mtukufu wa Makka, ambao anaushuhudia utukufu wake mwenye kwenda uzuru, na anapata amani mwenye kuuingia.
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِيٓ أَحۡسَنِ تَقۡوِيمٖ
Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa. [4]
[4] Kwa hakika bila ya shaka yoyote Sisi tumemuumba mtu amesimama sawa kwa umbo bora kabisa lilio nyooka, na akasifika kwa sifa nzuri kabisa.
ثُمَّ رَدَدۡنَٰهُ أَسۡفَلَ سَٰفِلِينَ
Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini! [5]
[5] Kisha tukamteremsha cheo mpaka akawa ni wa chini kabisa katika hao walioko chini, kwa kuacha kufanya waajibu wa hayo tuliyo muumbia.
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَلَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونٖ
Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha. [6]
[6] Lakini walio amini na wakatenda vitendo vyema, hao basi watapata ujira usio wakatikia wala kuwapungukia.
فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعۡدُ بِٱلدِّينِ
Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo? [7]
[7] Basi kitu gani kinacho kupelekea kukadhibisha kufufuliwa na kulipwa baada ya kuwekwa wazi uweza wetu wa hayo?
أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَحۡكَمِ ٱلۡحَٰكِمِينَ
Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote? [8]
[8] Kwani Mwenyezi Mungu aliye yatenda hayo tuliyo kueleza si muadilifu kuliko mahakimu wote kwa kufanya na kupanga?
At-Tin
Play