Surah An-Nas in Swahili

    الناس

    Surah An-Nas in Swahili

    Read Surah An-Nas in Swahili (الناس) with Arabic text, Swahili translation, and audio recitation. Chapter 114 of the Holy Quran, 6 verses — free online.

    Quran in Swahili · all 114 Surahs

    1

    قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ

    Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa wanaadamu, [1]

    [1] Sema: Najikinga na Mola Mlezi wa wanaadamu, Mwenye kuendesha mambo yao.

    2

    مَلِكِ ٱلنَّاسِ

    Mfalme wa wanaadamu, [2]

    [2] Mfalme wa wanaadamu, kwa ufalme ulio timia, kuwamiliki wote wafalme wao na maraia.

    3

    إِلَٰهِ ٱلنَّاسِ

    Mungu wa wanaadamu, [3]

    [3] Mungu wa wanaadamu, Mwenye uweza kwa kuwasarifu kwa ukamilifu atakavyo.

    4

    مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ

    Na shari ya wasiwasi wa Shetani, Khannas, [4]

    [4] Na shari ya mwenye kutia wasiwasi watu, ambaye hurudi nyuma ukiomba msaada kwa Mwenyezi Mungu dhidi yake.

    5

    ٱلَّذِي يُوَسۡوِسُ فِي صُدُورِ ٱلنَّاسِ

    Anaye tia wasiwasi katika vifua vya watu, [5]

    [5] Ambaye hutia kwa kificho katika vifua vya watu ya kuwaachisha wasende kwenye njia ya uwongofu.

    6

    مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ

    Kutokana na majini na wanaadamu. [6]

    [6] Kutokana na majini na wanaadamu.

    An-Nas

    Play