Surah Al-Masad in Swahili

    المسد

    Surah Al-Masad in Swahili

    Read Surah Al-Masad in Swahili (المسد) with Arabic text, Swahili translation, and audio recitation. Chapter 111 of the Holy Quran, 5 verses — free online.

    Quran in Swahili · all 114 Surahs

    1

    تَبَّتۡ يَدَآ أَبِي لَهَبٖ وَتَبَّ

    Imeangamia mikono ya Abu Lahab, na yeye pia ameangamia. [1]

    [1] Imeteketea mikono ya Abu Lahab iliyo kuwa ikiwaudhi Waislamu, na yeye mwenyewe amehiliki pia.

    2

    مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ

    Hayatamfaa mali yake, wala alivyo vichuma. [2]

    [2] Hayatolindwa na adhabu ya Mwenyezi Mungu mali yake aliyo kuwa nayo, wala cheo chake alicho kichuma.

    3

    سَيَصۡلَىٰ نَارٗا ذَاتَ لَهَبٖ

    Atauingia Moto wenye mwako. [3]

    [3] Ataingia katika Moto unao waka, aungue.

    4

    وَٱمۡرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ

    Na mkewe, mchukuzi wa kuni, [4]

    [4] Na ataingia pia kwenye Moto mkewe huyo aliye kuwa akibeba masengenyo baina ya watu, kama alivyo ingia yeye (mumewe).

    5

    فِي جِيدِهَا حَبۡلٞ مِّن مَّسَدِۭ

    Shingoni mwake iko kamba iliyo sokotwa. [5]

    [5] Juu ya shingo yake itakuwa kamba ya mtende ya kumtesa.

    Al-Masad

    Play