Surah Al-Qariah in Swahili

    القارعة

    Surah Al-Qariah in Swahili

    Read Surah Al-Qariah in Swahili (القارعة) with Arabic text, Swahili translation, and audio recitation. Chapter 101 of the Holy Quran, 11 verses — free online.

    Quran in Swahili · all 114 Surahs

    1

    ٱلۡقَارِعَةُ

    Inayo gonga! [1]

    [1] AL-QAARIA'H, Inayo gonga, ni Kiyama, ambacho kinaanza kwa mpulizo wa mwanzo wa barugumu, na kinaishia itapo katwa hukumu baina ya watu.

    2

    مَا ٱلۡقَارِعَةُ

    Nini Inayo gonga? [2]

    [2] Kitu gani kilicho cha ajabu zaidi katika ukuu wake, na khatari zake na kitisho chake!

    3

    وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ

    Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga? [3]

    [3] Na kitu gani kitacho kujuulisha hali ya AL-QAARIA'H katika kitisho chake juu ya nafsi za watu?

    4

    يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ

    Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika; [4]

    [4] Siku hiyo watu watakuwa kama vipepeo kwa wingi na kuhangaika kulia na kushoto, madhaifu na wanyonge!

    5

    وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ

    Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa! [5]

    [5] Na milima itakuwa kama sufi iliyo tiwa rangi na kuchambuliwa kwa kutapanyika vipande mbali mbali na kupeperuka katika anga huku na huku.

    6

    فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ

    Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, [6]

    [6] Ama yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, mema yake yakapindukia kuliko maovu yake,

    7

    فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ

    Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza. [7]

    [7] Basi huyo atakuwa na maisha yatayo mridhisha mwenyewe, na nafsi yake itue.

    8

    وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ

    Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, [8]

    [8] Na ama ambaye mizani yake itakuwa nyepesi, na maovu yake yakazidi kuliko mema yake,

    9

    فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ

    Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya! [9]

    [9] Basi makaazi yake yatakuwa Jahannamu.

    10

    وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ

    Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo? [10]

    [10] Na nini cha kukujuulisha ni nini Hawiya?

    11

    نَارٌ حَامِيَةُۢ

    Ni Moto mkali! [11]

    [11] Moto ulio mkali, hapana moto unao fikilia ukali wake, hata ukichochewa vipi na kutiwa kuni gani!

    Al-Qariah

    Play