أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يُكَذِّبُ بِٱلدِّينِ
Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo? [1]
[1] Unamjua anaye kanusha malipo na hisabu ya Akhera?
الماعون
Read Surah Al-Maun in Swahili (الماعون) with Arabic text, Swahili translation, and audio recitation. Chapter 107 of the Holy Quran, 7 verses — free online.
Quran in Swahili · all 114 Surahs
أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يُكَذِّبُ بِٱلدِّينِ
Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo? [1]
[1] Unamjua anaye kanusha malipo na hisabu ya Akhera?
فَذَٰلِكَ ٱلَّذِي يَدُعُّ ٱلۡيَتِيمَ
Huyo ndiye anaye msukuma yatima, [2]
[2] Ukitaka kumjua basi ni huyo ambaye anaye msukuma yatima kwa nguvu, na anamtumilia mabavu, na anamdhulumu,
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hahimizi kumlisha masikini. [3]
[3] Na wala hahimizi kulishwa masikini.
فَوَيۡلٞ لِّلۡمُصَلِّينَ
Basi, ole wao wanao swali, [4]
[4] Maangamio yatawashukia wanao sali na wakasifika kwa sifa hizi, na wakaghafilika na Swala zao wasinafiike nazo.
ٱلَّذِينَ هُمۡ عَن صَلَاتِهِمۡ سَاهُونَ
Ambao wanapuuza Sala zao; [5]
[5] Maangamio yatawashukia wanao swali na wakasifika kwa sifa hizi, na wakaghafilika na Swala zao wasinafiike nazo.
ٱلَّذِينَ هُمۡ يُرَآءُونَ
Ambao wanajionyesha, [6]
[6] Ambao huonyesha kwa watu vitendo vyao, ili wapate cheo katika nyoyo za hao watu, na wasifiwe.
وَيَمۡنَعُونَ ٱلۡمَاعُونَ
Nao huku wanazuia msaada. [7]
[7] Na huku wanazuia hisani zao na msaada wao kwa watu
Al-Maun
Play